Friday, April 20, 2012

Soma Qur'an Tuifahamu Dini yetu(25:3)


QUR'AN NI KITABU (2:2) na ni MUUJIZA ulio HAI - KISOMWI kilichotakaswa (98:2) Nuru ambayo kwayo (Allah) Humuongoza Amtakaye (42:52).
Ni agizo kwetu kuisoma (73:4) kwani ni ukumbusho kwa walimwengu wote (69:70) Hasa kwa yule anayetaka kushika njia (81:27-28) yakurejea kwa Mola wake (42:10).
Na Kitabu (hiki) hakikutemremshiwa (Mtume Muhammad) isipokuwa abainishie (watu) yale ambayo (1) Wanakhilitilafiana na (kiwe) (2) uongozi na (3) rehema kwa watu wanaoamini (16:64) ili Dini ihuishwe (16:65) kwa amri yake (na) watu waonyeke kuwa hakuna kiongozi ila Yeye (Allah), basi Aogopwe (16:2) Yeye tu. Yeye ndiye mwenye vyeo vya juu, Mwenyekiti (40:15) Kiongozi (wetu) mmoja tu (37:4), Rais wa mbingu na ardhi na yaliyomo kati yake; na ni Rais wa (nchi zote zilizoko) mashariki (na zilizoko Magharibi) (37:5).
Rais wetu huyu (Allah) Ametufanyia hisani kubwa waumini (vile) alivyomleta Mtume akatusomea Aya zake, na kututakasa na kutufundisha Kitabu na hikima (3:164), (ili tusalimike na) upotofu (huu tulionao sasa duniani) ulio dhahiri (3:164). Upotofu huu uliodhahiri ni kule kushika miungu mingine badala yake (36:23-24). Na miungu hiyo si wengine bali ni Viongozi bandia (wanaofarikiana 12:39) tuliowateka (15:96) na kuwapa vyeo (majina) tunavyopanga sisi wenyewe (12:40) pindi walipohitimu katika vyuo vikuu (9:31). Hivyo wao wanavyuoni wetu hawa na watawa (lao moja), wametuwekea dini (isiyokuwa ndiyo) (42:21) tulipowafanya sawa na Rais (Mola) wa walimwengu wote tulipowateua kuwa viongozi (26:98). Imekuaje tumegeuzwa (10:32) na kuingizwa kwenye upotofu kwa kumuweka Rais (Mola) wetu wa Kweli Allah? (10:31). Kiongozi anayeturuzuku kutoka mbinguni na katika ardhi, sio kutupeleka kuomba misaada kwa wazungu na kwa wachina 22:13) anayemiliki masikio na macho, amtoaye mzima katika mfu na kumtoa mfu katika mzima. Na hutengeneza mambo yote (10:31). Imekuwaje? Hatusadiki (10:31) hivyo tungojee kuthubutikiwa na kauli yake kwa kuasi kwetu? (10:33). La!
(Muhammad) alitumwa (kuja) kuongoza na (kutufunza) dini ya haki (chama cha kweli) ili aijaalie kushinda (kuchukua uongozi chama hiki) juu ya dini zote (vyama vyote); ijapokuwa watachukia MADEMOKRATI (WASHIRIKINA 30:31-32) (9:33). Kumbe neno washirikina limebatizwa na kuitwa mademokrati bila sisi kujua utaratibu wa maisha unajaalia watu kukhitilafiana.

IKHTILAFU:
Muhammad (47) kaletwa kubainisha Ikhtilafu iliyoko baina ya watu kwa wale wanaoamini (16:64) (wanaofuata aya za Allah 28:47).
Tujiulize ni nini Ikhtilafu? Jibu: Kwa wale wanaofuata Aya za Allah (28:47) Ikhtilafu ni ile Khabari Kubwa (78:2-3).
Kuwa macho ( ). Yaliyosemwa hapo ni kwamba, kwa wale waumini (28:47) wao Ikhtilafu ni ile Khabari Kubwa. Na nini basi kitakachokujulisha (90:12) hata akajua KHABARI KUBWA ni nini Jibu:
KHABARI KUBWA (38:67) ni yule mwingi wa Rehema, mwenye nguvu, Rais wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake (38:66) Mmoja hakuna Kiongozi (Mungu) ila Yeye (38:65) Hivyo tuonyeke (25:1) kwamba Umma wetu huu ni Umma mmoja, na yeye (Allah) ni Rais wetu (21:92). (Lakini) jambo hili tumejiepusha nalo (38:68) na kulivunja baina yetu (tukafarikiana (21:93) na kuwa makundi makundi (30:53). Hivyo tumeshika miungu (viongozi) wengine badala Yake (42:9),

WITO WA MUHAMMAD
Mlinganiaji wa Allah akiita (46:31) "Enyi watu! Njooni katika neno lililosawa ....., ya kwamba:
1. Tusimuheshimu, wala kumuogopa wala kumuomba, wala kumpenda kupita kiasi [taz: Kamusi neno Abudu (kd)] yeyote yule ila Allah; wala tusimshirikishe na chochote (tusifuate matamanio ya nafsi 45:23); tusije wafanya wengine (wetu) kuwa viongozi badala ya Allah (nao ni wanavyuoni na watawa ambao tunawapigia kura) 3:64 kutomuitikia mlingani huyu (tukadai kuwa maongozi yetu haya, hayana dini); ndio kuwa katika upotofu uliodhahiri (46:32) Na jambo hili la kukataa uungu (Uongozi) wa Kiongozi mmoja ndio "Munkar" (16:22). "Munkari: uzuiliwe (ukataze (3:114), Eh!
Uongozi wa Allah ndio Uongozi (2:120) Kwa hiyo ikisemwa MUNKARI UZUILIWE, moja ya maana ni kwamba usiwepo Uongozi mwingine bighairi ya huu wa Allah. Jambo la leadership (uwongozi) ni wa nani; mtu asishindane nawe. Na walinganie watu kumwendea (kumwelekea kwa maongozi) Rais wako. Bila shaka wewe (Muhammad) uko juu ya uongozi ulio na msimamo (22:67-68). Mwenyezi Mungu anajua yote (wapinzani 38:2) wanayoyatenda (22:69), Hukumu ni Yake siku ya kiama katika Ikhtilafu (hii) (22:69) ya kumpa ukuu na ukubwa binadamu wenzetu tukawafuata (33:47) badala ya Allah ambaye ndiye Mkubwa na ndiye aliye juu, juu, juu, zaidi.(2:255).

Kumuabudu Allah:
LENGO la watu kuumbwa ni ili tupate kumuabudu (51:56) (Allah). Kumuabudu Allah, ndio njia iliyonyooka (43:64). Na kwa kushika yaliyofunuliwa kwa Muhammad (43:43) nayo ni kwamba hakuna kiongozi ila kiongozi mmoja tu (21:108), itapelekea kuwa katika njia iliyonyooka (43:43) ambayo yeye Muhammad aliongoza kwayo (42:52) nayo ndiyo njia ya Allah (42:53). Uislamu (6:126) dini ya Mitume wote (42:13)Amri (45:17) kumi za Nabii Musa ni njia ya Muhammad iliyonyooka (6:151-153). Dini hii ndio Allah aliyotuchagulia (2:132) (aliyotusajilia) na kutupendelea (5:3) (kutupa kibali). Kwa hiyo tusife isipokuwa tumeshakuwa Waislamu.
Waislamu ni watu ambao humuheshimu na kumuogopa na kumuomba na kumpenda kupita kiasi kiongozi (Mungu) mmoja tu, kiongozi (Mola) wa mababu zetu waliotutangulia (2:133). Lakini kwa kuwaheshimu na kuwaomba na kuwaogopa na kuwapenda kupita kiasi badala ya Allah (miungu) ambayo haikuteremshia amri na ambayo hatuna ilimu nayo (22:71), wametupambia kuwaua watoto (uzazi wa majira) na dini (utaratibu wa maisha) kuvurugika (6:137). Hivyo kufarakana kwetu katika dini na kuwa makundi makundi tujue hivyo hatuna uhusiano na Muhammad (6:159)
Waislamu si wengine bali ni wale watu wanaoamini aya za Allah (27:81). Wao humwogopa na kumuomba na kumheshimu na kumpenda kupita kiasi (humuabudu Rais wa mjia (wa Makka) (27:91). Kwani Makka ndio mji wao mkuu (Kibla) (2:150) wanaelekea kwa maongozi na baraka (3:96). Muhammad ndiye Mbunge (Nabii) wao wanayemfuata (2:143) kwa sababu Rais (Mola) wao ni Allah (22:40).
Na dini yao (chama) ni Uislamu (41:33). Kitabu chao (katiba) ni Qur'an (27:92). Ifuatwe Katiba hii bila kuzuiwa na yeyote na kampeni ifanyike (28:87) ili watu wamjue Rais wao wa kweli. Namna hivi aya zinaelezwa (6:55) ili (watu) wapate kufahamu (6:65). Na ili njia ya waovu (Marais) ibainike (6:55).
Tumeona kuwa Waislamu ni wale wenye kuamini aya zake Allah (27:81) nazo ni kitabu (13:1) Qur'an aliyoifundisha (55:2) sasa ni nini kitakachokujulisha hata ukajua (kuamini kitabu 2:177) ni kitu gani? Allah anajibu kwa kusema:
"Hakika wanaoamini aya zetuni wale tu ambao wanapokumbushwa nazo huanguka kusujudu, na humtukuza Mola wao kwa kutaja sifa zake, nao hawatakabari (32:15). Huinuka mbavu zao kutoka vitandani wakati wa usiku ili kumuomba Mola wao kwa kuogopa moto na kutaraji pepo na hutoa katika yale tuliowapa (32:16). Mwenye sifa hizi ndiye ambaye kwa lugha ya Kiarabu na sasa Kiswahili huitwa Muislamu.


Uongozi:
Yeye Muhammad kaletwa kutubainishia uongozi (16:64) wa kutiiwa ulio na matokeo bora (maendeleo) (4:59). Kwani suala la uongozi ni jukumu lake (Allah) (92:12). Humuongoza amtakaye (2:272) naye akamteremsha (wanaotaka) kuongozwa (28:56). Hivyo akamteremshia kitabu (18:1-5). Kwa kitabu hicho Allah huwaongoza wenye kufuata radhi yake katika njia za salama (sio njia za upinzani), na huwatoa katika dhulma (shirki 31:13) kuwapeleka katika nuru kwa idhini yake na kuwaongoza katika njia iliyonyoka (5:16)


Uongozi ni nini?
Uongozi si mtu bali ni nyumba (inayoendewa) (5:2) kutafuta fadhila za Rais wao na radhi yake (5:2) (Na zingatia uone kwamba wenye kutafuta fadhila na radhi za kiongozi wao huyo) hupeleka katika nyumba hiyo wanyama wakachinjwe (5:2).
(Kumbuka) mababu zetu waliyaendea mapango au misitu (sehemu za faragha walizoziteua na kuziheshimu) (5:2) na waliandamana nao wanyama wa kuchinjwa (tambiko au kafara) (5:2) na walisaidiana kwa (wema 2:177) na hofu wala hawakusaidiana katika dhambi na uadui (5:2). Wakamlilia (Rais Muumba 39:6) wao kwa shida na matatizo yao. Kauli zao ilikuwa kitu kama hii:
"Eh!Mfalme Mungu - Mungu wa Babu zetu Kajia, Kajiru na Kisumo (linganisha 2:133) ni wewe tu tunayekujua unayetipisha jua angani - tusikie kwani sisi ni wajukuu wao - tumekukosea tu- tumekuja kukuomba".
Na wazee wetu walichokiomba hasa ilikuwa; mvua, kueupushwa na maradhi na watoto (19:5).
Hebu tuone wakati wetu huu: Zingatia kuwa kuta za mapango ni majabali. Je! Huoni kwamba sisi tulichofanya ni kuyaendea mapango (majabali) na kuyavunja vunja. Halafu tukahamisha mapango haya na kuyajenga mjini? Mara tukayabandika jina "nyumba" badala ya kuyaita "mapango ya kisasa". Na humo tukaweka vyumba, vikaitwa ofisi. Na ni ofisini humo tukajaalia (15:96) wenzetu kukaa humo kusimamia uwongozi wa katiba tuliyounda wenyewe. Tukawafanya viongozi (18:102) na wana majina kibao (12:40) kufuatana na wadhifa waliosomea.
Oh! Tuna shida na tatizo sasa. Moja kwa moja huyaendea mapango haya ya kisasa (1) ofisi ya chama au serikali kuomba fadhila ( kama maji) za viongozi tuliowasilimika. Na ili tupate Radhi zao lazima tutoe kitu kidogo (chakula cha mgeni rasmi na vinywaji). Kama shida hiyo ni ugomvi au kudhulumiana huenda kituo (nyumba) cha polisi - huyo Mahakamani. Kama ni maradhi huenda hospitali na kadhalika.
Na kote huko si bure ili upate fadhila (huduma) na radhi zao (msaada) lazima utoe hongo. Mfano utakuta watoza ushuru (wenye kuzitumikia 9:60) anakuambia ah! Ushuru wako ni milioni tatu. Una uwezo wa kulipa?
Sasa wewe pale unajililia eti akusaidie. Basi wewe unampa milioni moja lakini anakuandikia risiti ya laki nne. Ajabu nani amemsaidia mwenzake! Yeye au wewe?
Yote ni mamoja. Hawa tunaowamba wanahitajia vitu kwetu. Na kweli tumekuwa watumwa wao. Hapana maongozi ya mapango ya kisasa (ofisi za chama na serikali) ni dini hiyo. Utajuwaje?
Watu husema dini ni imani. Ikiwa imani ni dini basi jua kuwa ukisema ujamaa ni imani, umesema kuwa ujamaa ni dini. Na hapa ndipo kosa lilipozaliwa. Tukawa wenye makosa (khatiya). Kosa lenyewe ni hili:
Imani yetu hii kwa mfano ujamaa tuliyopambwa nayo nyoyoni mwetu tukaipenda na kuitia (kumbuka seti Benjamin); tuliichukua kutoka kwenye pango la kisasa (ofisi) la chama tawala. Ili hali Rais wetu wa ulimwengu mzima (1:1) ametuagiza wanadamu wote tukuchue mapambo yetu kutoka Misikitini (kwenye masinagogi) (7:31).


Pambo ni nini?
Sura ya 49 aya ya saba inatufahamisha kuwa kilichopendezeshwa kwetu ni imani na ndilo pambo la moyoni. Na usije kufa kabla hujalivaa pambo hilo (3:102). Kwa hiyo imani yetu twatakiwa kuichukua kutoka kwenye pango la kisasa liitwalo Msikiti (7:31) na sio ofisi. Jua kila ofisi ina katiba yake iliyoundwa na watu. Kwa hiyo maongozi yake ni ya kubuniwa na watu. Bali Msikiti nao unayo kitabu (katiba). Na kitabu hiki ni cha Rais wetu Allah (112:1) mmoja. Kwa katiba hiyo kufuatwa itapelekea kufuata maongozi ya Allah (5:16) ili atuongoze katika njia iliyonyooka (4:175), dini yetu aliyoisajili na kutupa kibali jinale Uislamu (5:3).


Kibla
Neno Kibla maana yake ni upande (2:177) unaoelekewa (2:150) kwa maongozi (3:96). Ajabu majumba haya ya Allah (72:18) (Misikiti) yote dunia nzima yameelekea (nyumba kongwe 22:29). Na huu ndio ukombozi wetu (nyumba tukufu 5:97) Rais wetu Allah (ameifanya 5:97) mji wa Makka ndio mji mkuu (mama wa miji) miji yote duniani ielekee huko (6:92).
Humo kipo kitabu (katiba) chenye baraka (9:62). Kwa hayo jua kuwa ofisi (Pango la kisasa) halali kuendewa kwa utatuzi wa shida na matatizo ya watu ni Msikiti. Yenyewe Misikiti hii imeelekezwa Makka. Nasi tuelekeze nyuso zetu huko (2:148, 150, 144, 143, 145) kwani hiyo ndiyo haki iliyotoka kwa Rais (Mola) wetu (2:147) na ndiyo aliyoteremshiwa Muhammad (13:1) na ndilo agizo aliloagizwa kufikisha (5:67).

Na: Tahir Rashid

No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget